Wasimamizi Wa Idara Ndani Ya Kanisa


  1. Idara ya Vijana               [Alex Mkandawile, +255713969152]
  2. Idara ya Wakinababa      [Geofrey Mwesiga, +255742437602]
  3. Idara ya Wakinamama    [Mch. Sophia Sarungi ,+255657483150]
  4. Idara ya Uinjilist             [Obedi Mwakapiki, +255685316601]  
  5. Idara ya watoto

: IDARA MBALIMBALI NDANI YA GROWING MISSION CHURCH. 
➢ Kanisa hili litakuwa na idara mbalimbali kama ifuatavyo: 

IDARA YA WAMAMA 
➢ Idara hii itajulikana kwa jina la Wanawake Jeshi Kubwa kwa kifupi chake W.J.K. Kazi ya idara ya wamama: 
1. Ni kusimamia malengo ya idara ya wanawake 
2. kuona kwamba akina mama wanaongozwa katika misingi ya kiroho pamoja na kutunza watoto wao vizuri.
 3. Kuhakikisha kwamba wakina mama nao wanajihusisha katika kueneza kazi ya Mungu. 16 

IDARA YA VIJANA (CAIM) 
➢ Idara hii itajulikana kwa jina la Mabalozi wa Huduma ya Kristo (Christ Ambassadors in Mission) kwa kifupi MHK ( CAIM) Kazi ya Idara ya vijana (CAIM) 
1. Kuwasaidia vijana kwa njia ya mafundisho ili wakue katika hali ya kumcha Mungu 
2. Kuwasaidia vijana kusudi wajue jinsi ya kushuhudia Neno la Mungu mitaani/sokoni/Hospitalini/Magerezani/shuleni/na mikutano ya hadhara. 
3. Kuwafanya vijana wajue jinsi ya kutegemeza makanisa/shule/za Biblia kwa fedha zao na maombi yao. 
4. Kuwaunganisha vijana wa kanisa letu nchi nzima na kushirikiana na vijana wenye imani sawa na yetu ulimwenguni.
 5. Kuwasaidia vijana kwa hali na mali wakati wanapofikia kuoa au kuolewa 

IDARA YA WABABA (WWN )
 Idara hii itajulikana kwa jina la Wababa ni Watendaji wa Neno Kazi ya idara ya wababa
 1. Ni kusimamia malengo ya idara ya wababa
 2. kuona kwamba akina baba wanaongozwa katika misingi ya kiroho pamoja na kutunza familia zao vizuri, yaani mke na watoto.
 3. Kuhakikisha kwamba wakina baba nao wanajihusisha katika kueneza kazi ya Mungu, kama Wababa watendaji wa Neno lilivyo.

 IDARA YA WATOTO ( HUWK )
 Hii ni idara muhimu sawa na idara nyingine katika kanisa yenye lengo la kutoa elimu ya Biblia kanisani kwa kila mkristo. Kwa kifupi itaitwa Huduma ya Uangalizi wa Watoto wa Kikristo (HUWK) Kazi yake:- ( Mithali 22:6 na Mithali 4:13)
 1. Ni kufundisha Sunday school ukizingatia sana Neno la Mungu kuanzia Agano la kale na Agano jipya ili kuhakikisha kwamba Biblia nzima inafundishwa kwa wanafunzi wa rika zote (kanisa). 17 
2. Waalimu wa shule hii ya Jumapili lazima wawe ni wakristo wanaoelewa vizuri Neno la Mungu na wawe na uwezo wa kufundisha wengine. 
3. Mchungaji au Baraza la wazee wahakikishe kuwa walimu hao wana maisha safi ya kiroho na elimu inayokubalika na nchi yetu. Isaya 52:11c